Zaburi Chapter 71

For English

Read Zaburi Chapter 71 Online

Read Zaburi Chapter 71 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of Zaburi in the Old Testament. Browse every verse with easy chapter navigation, continue to the next chapter, or explore the complete Book of Zaburi and the Holy Bible online.

Choose a Chapter

Zaburi 71

Sura 71

1. Nimekukimbilia Wewe, Bwana, Nisiaibike milele.

2. Kwa haki yako uniponye, uniopoe, Unitegee sikio lako, uniokoe.

3. Uwe kwangu mwamba wa makazi yangu, Nitakakokwenda sikuzote. Umeamuru niokolewe, Ndiwe genge langu na ngome yangu.

4. Ee Mungu wangu, uniopoe mkononi mwa mkorofi, Katika mkono wake mwovu, mdhalimu,

5. Maana ndiwe taraja langu, Ee Bwana MUNGU, Tumaini langu tokea ujana wangu.

6. Nimekutegemea Wewe tangu kuzaliwa, Ndiwe uliyenitoa tumboni mwa mama yangu, Ninakusifu Wewe daima.

7. Nimekuwa kitu cha ajabu kwa watu wengi, Na Wewe ndiwe kimbilio langu la nguvu.

8. Kinywa changu kitajazwa sifa zako, Na heshima yako mchana kutwa.

9. Usinitupe wakati wa uzee, Nguvu zangu zipungukapo usiniache.

10. Kwa maana adui zangu wananiamba, Nao wanaoniotea roho yangu hushauriana.

11. Wakisema, Mungu amemwacha, Mfuatieni, mkamateni, hakuna wa kumponya.

12. Ee Mungu, usiwe mbali nami; Ee Mungu wangu, fanya haraka kunisaidia.

13. Waaibishwe, watoweshwe, adui za nafsi yangu. Wavikwe laumu na aibu wanaonitakia mabaya.

14. Nami nitatumaini daima, Nitazidi kuongeza sifa zake zote.

15. Kinywa changu kitasimulia haki na wokovu wako Mchana kutwa; maana sijui hesabu yake.

16. Nitakuja na mambo ya ajabu ya Bwana MUNGU; Nitawakumbusha watu haki yako Wewe peke yako.

17. Ee Mungu, umenifundisha tokea ujana wangu; Nimekuwa nikitangaza miujiza yako hata leo.

18. Na hata nikiwa ni mzee mwenye mvi, Ee Mungu, usiniache. Hata niwaeleze watu wa kizazi hiki nguvu zako, Na kila atakayekuja uweza wako.

19. Na haki yako, Ee Mungu, Imefika juu sana. Wewe uliyefanya mambo makuu; Ee Mungu, ni nani aliye kama Wewe?

20. Wewe, uliyetuonyesha mateso mengi, mabaya, Utatuhuisha tena. Utatupandisha juu tena Tokea pande za chini ya nchi.

21. Laiti ungeniongezea ukuu! Urejee tena na kunifariji moyo.

22. Nami nitakushukuru kwa kinanda, Na kweli yako, Ee Mungu wangu. Nitakuimbia Wewe kwa kinubi, Ee Mtakatifu wa Israeli.

23. Midomo yangu itafurahi sana nikuimbiapo, Na nafsi yangu uliyoikomboa.

24. Ulimi wangu nao utasimulia Haki yako mchana kutwa. Kwa maana wameaibishwa, Wametahayarika, wanaonitakia mabaya.

About Zaburi Chapter 71

Read Zaburi Chapter 71 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of Zaburi in the Old Testament. Continue reading with the chapter navigation above or explore the complete book.

Book Information

Book: Zaburi
Chapter: 71
Testament: Old Testament

How to Read this Chapter

Use the Previous and Next Chapter buttons to continue reading Zaburi. You can also adjust the font size for comfortable reading and browse other books of the Bible using the navigation links.

https://www.youtube.com/watch?v=rzsT_Q3KLzE

More Resources

Continue Reading the Bible

Continue reading Zaburi Chapter 71 and explore every book, chapter and verse of the Holy Bible. Use the navigation links above and below to move through the Scriptures with ease.

Frequently Asked Questions

What is Zaburi Chapter 71?

Zaburi Chapter 71 is part of the Book of Zaburi in the Holy Bible.

Can I read this chapter online?

Yes. You can read the complete Zaburi Chapter 71 online for free with easy chapter navigation.

More Chapters from Agano la Kale

  1. Zaburi Chapter 1
  2. Habakuki Chapter 3
  3. Ayubu Chapter 1
  4. Zaburi Chapter 2
  5. Kutoka Chapter 11
  6. Kutoka Chapter 2
  7. Ayubu Chapter 4

Explore More from Zaburi

  1. Zaburi Chapter 12
  2. Zaburi Chapter 17
  3. Zaburi Chapter 98
  4. Zaburi Chapter 57
  5. Zaburi Chapter 122
  6. Zaburi Chapter 13
  7. Zaburi Chapter 148

Related Chapters & Readings

  1. Ezra Chapter 6
  2. 2 Samweli Chapter 9
  3. Zaburi Chapter 84
  4. Wagalatia Chapter 4
  5. Mhubiri Chapter 9
  6. Mwanzo Chapter 32
  7. Zaburi Chapter 127
Share Your Love

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *