Zaburi Chapter 69

For English

Read Zaburi Chapter 69 Online

Read Zaburi Chapter 69 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of Zaburi in the Old Testament. Browse every verse with easy chapter navigation, continue to the next chapter, or explore the complete Book of Zaburi and the Holy Bible online.

Choose a Chapter

Zaburi 69

Sura 69

1. Ee Mungu, uniokoe, Maana maji yamefika mpaka nafsini mwangu.

2. Ninazama katika matope mengi, Pasipowezekana kusimama. Nimefika penye maji ya vilindi, Mkondo wa maji unanigharikisha.

3. Nimechoka kwa kulia kwangu, Koo yangu imekauka. Macho yangu yamedhoofu Kwa kumngoja Mungu wangu.

4. Wanaonichukia bure ni wengi Kuliko nywele za kichwa changu. Watakao kunikatilia mbali wamekuwa hodari, Adui zangu kwa sababu isiyo kweli. Hata mimi nalilipishwa kwa nguvu Vitu nisivyovichukua.

5. Ee Mungu, unajua upumbavu wangu, Wala hukufichwa dhambi yangu.

6. Wanaokungoja Wewe wasiaibishwe, Kwa ajili yangu, Bwana, MUNGU wa majeshi. Wanaokutafuta Wewe wasifedheheshwe, Kwa ajili yangu, Ee Mungu wa Israeli.

7. Maana kwa ajili yako nimestahimili laumu, Fedheha imenifunika uso wangu.

8. Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, Na msikwao kwa wana wa mama yangu.

9. Maana wivu wa nyumba yako umenila, Na laumu zao wanaokulaumu zimenipata.

10. Nilipolia na kuiadhibu roho yangu kwa kufunga, Ikawa laumu juu yangu.

11. Nilipofanya gunia kuwa nguo zangu, Nikawa mithali kwao.

12. Waketio langoni hunisema, Na nyimbo za walevi hunidhihaki.

13. Nami maombi yangu nakuomba Wewe, Bwana, Wakati ukupendezao; Ee Mungu, Kwa wingi wa fadhili zako unijibu, Katika kweli ya wokovu wako.

14. Uniponye kwa kunitoa matopeni, Wala usiniache nikazama. Na niponywe nao wanaonichukia, Na katika vilindi vya maji.

15. Mkondo usinigharikishe, wala vilindi visinimeze, Wala shimo lisifumbe kinywa chake juu yangu.

16. Ee Bwana, unijibu, maana fadhili zako ni njema, Kwa kadiri ya rehema zako unielekee.

17. Wala usinifiche uso wako, mimi mtumishi wako, Maana mimi nimo taabuni, unijibu upesi.

18. Uikaribie nafsi yangu, uikomboe, Kwa sababu ya adui zangu unifidie.

19. Wewe umejua kulaumiwa kwangu, Na kuaibika na kufedheheka kwangu, Mbele zako Wewe wako watesi wangu wote.

20. Laumu imenivunja moyo, Nami ninaugua sana. Nikangoja aje wa kunihurumia, wala hakuna; Na wa kunifariji, wala sikumwona mtu.

21. Wakanipa uchungu kuwa chakula changu; Nami nilipokuwa na kiu wakaninywesha siki.

22. Meza yao mbele yao na iwe mtego; Naam, wakiwa salama na iwe tanzi.

23. Macho yao yatiwe giza wasione, Na viuno vyao uvitetemeshe daima.

24. Uimwage ghadhabu yako juu yao, Na ukali wa hasira yako uwapate.

25. Matuo yao na yawe ukiwa, Pasiwe na mtu wa kukaa hemani mwao.

26. Maana wanamwudhi mtu uliyempiga Wewe, Wanasimulia maumivu ya hao uliowatia jeraha.

27. Uwaongezee uovu juu ya uovu, Wala wasiingie katika haki yako.

28. Na wafutwe katika chuo cha uhai, Wala pamoja na wenye haki wasiandikwe.

29. Nami niliye maskini na mtu wa huzuni, Mungu, wokovu wako utaniinua.

30. Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo, Nami nitamtukuza kwa shukrani.

31. Nayo yatampendeza Bwana kuliko ng'ombe, Au ndama mwenye pembe na kwato.

32. Walioonewa watakapoona watafurahi; Enyi mmtafutao Mungu, mioyo yenu ihuishwe.

33. Kwa kuwa Bwana huwasikia wahitaji, Wala hawadharau wafungwa wake.

34. Mbingu na nchi zimsifu, Bahari na vyote viendavyo ndani yake.

35. Maana Mungu ataiokoa Sayuni, na kuijenga miji ya Yuda, Na watu watakaa ndani yake na kuimiliki.

36. Wazao wa watumishi wake watairithi, Nao walipendao jina lake watakaa humo.

About Zaburi Chapter 69

Read Zaburi Chapter 69 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of Zaburi in the Old Testament. Continue reading with the chapter navigation above or explore the complete book.

Book Information

Book: Zaburi
Chapter: 69
Testament: Old Testament

How to Read this Chapter

Use the Previous and Next Chapter buttons to continue reading Zaburi. You can also adjust the font size for comfortable reading and browse other books of the Bible using the navigation links.

https://www.youtube.com/watch?v=rzsT_Q3KLzE

More Resources

Continue Reading the Bible

Continue reading Zaburi Chapter 69 and explore every book, chapter and verse of the Holy Bible. Use the navigation links above and below to move through the Scriptures with ease.

Frequently Asked Questions

What is Zaburi Chapter 69?

Zaburi Chapter 69 is part of the Book of Zaburi in the Holy Bible.

Can I read this chapter online?

Yes. You can read the complete Zaburi Chapter 69 online for free with easy chapter navigation.

More Chapters from Agano la Kale

  1. Zaburi Chapter 1
  2. Habakuki Chapter 3
  3. Ayubu Chapter 1
  4. Zaburi Chapter 2
  5. Kutoka Chapter 11
  6. Kutoka Chapter 2
  7. Ayubu Chapter 4

Explore More from Zaburi

  1. Zaburi Chapter 115
  2. Zaburi Chapter 48
  3. Zaburi Chapter 104
  4. Zaburi Chapter 64
  5. Zaburi Chapter 33
  6. Zaburi Chapter 97
  7. Zaburi Chapter 66

Related Chapters & Readings

  1. Luka Chapter 6
  2. Mwanzo Chapter 13
  3. Zaburi Chapter 68
  4. Zaburi Chapter 60
  5. Matendo ya Mitume Chapter 13
  6. Luka Chapter 1
  7. Ezekieli Chapter 19
Share Your Love

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *