Mathayo Chapter 15

For English

Read Mathayo Chapter 15 Online

Read Mathayo Chapter 15 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of Mathayo in the New Testament. Browse every verse with easy chapter navigation, continue to the next chapter, or explore the complete Book of Mathayo and the Holy Bible online.

Choose a Chapter

Mathayo 15

Sura 15

1. Ndipo Mafarisayo na waandishi toka Yerusalemu walipomwendea Yesu wakisema,

2. Mbona wanafunzi wako huyahalifu mapokeo ya wazee, kwa maana hawanawi mikono walapo chakula.

3. Akajibu, akawaambia, Mbona ninyi nanyi huihalifu amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu?

4. Kwa kuwa Mungu alisema, Mheshimu baba yako na mama yako, na Amtukanaye baba yake au mama yake kufa na afe.

5. Bali ninyi husema, Atakayemwambia babaye au mamaye, Cho chote kikupasacho kusaidiwa na mimi ni wakfu,

6. basi asimheshimu baba yake au mama yake. Mkalitangua neno la Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu.

7. Enyi wanafiki, ni vema alivyotabiri Isaya kwa habari zenu, akisema,

8. Watu hawa huniheshimu kwa midomo; Ila mioyo yao iko mbali nami.

9. Nao waniabudu bure, Wakifundisha mafundisho Yaliyo maagizo ya wanadamu.

10. Akawaita makutano akawaambia

11. Sikilizeni, mfahamu; Sicho kiingiacho kinywani kimtiacho mtu unajisi; bali kitokacho kinywani ndicho kimtiacho mtu unajisi.

12. Ndipo wanafunzi wake walipomwendea, wakamwambia, Wajua ya kuwa Mafarisayo walipolisikia neno lile walichukizwa?

13. Akajibu, akasema, Kila pando asilolipanda Baba yangu wa mbinguni litang'olewa.

14. Waacheni; hao ni viongozi vipofu wa vipofu. Na kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, watatumbukia shimoni wote wawili.

15. Basi Petro akajibu, akamwambia, Tueleze mfano huo.

16. Yesu akasema, Hata sasa ninyi nanyi mngali hamna akili?

17. Hamjafahamu bado ya kuwa kila kiingiacho kinywani hupita tumboni, kikatupwa chooni?

18. Bali vitokavyo kinywani vyatoka moyoni; navyo ndivyo vimtiavyo mtu unajisi.

19. Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wivi, ushuhuda wa uongo, na matukano;

20. hayo ndiyo yamtiayo mtu unajisi; lakini kula kabla hajanawa mikono hakumtii mtu unajisi.

21. Yesu akaondoka huko, akaenda kando pande za Tiro na Sidoni.

22. Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo.

23. Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu.

24. Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.

25. Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie.

26. Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.

27. Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao.

28. Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, Mama, imani yako ni kubwa; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile.

29. Yesu akaondoka huko, akafika kando ya bahari ya Galilaya; akapanda mlimani, akaketi huko.

30. Wakamwendea makutano mengi wakimletea viwete, vipofu, mabubu, vilema, na wengine wengi, wakawaweka miguuni pake; akawaponya;

31. hata ule mkutano wakastaajabu, walipowaona mabubu wanasema, vilema wanakuwa wazima, viwete wanakwenda, na vipofu wanaona; wakamtukuza Mungu wa Israeli.

32. Yesu akawaita wanafunzi wake, akasema, Nawahurumia mkutano, kwa kuwa yapata siku tatu wamekaa pamoja nami, wala hawana kitu cha kula, tena kuwaaga wakifunga sipendi, wasije wakazimia njiani.

33. Wanafunzi wake wakamwambia, Tupate wapi mikate mingi hapa nyikani, hata kushibisha mkutano mkuu namna hii?

34. Yesu akawaambia, Mnayo mikate mingapi? Wakasema, Saba, na visamaki vichache.

35. Akawaagiza mkutano waketi chini;

36. akaitwaa ile mikate saba na vile visamaki, akashukuru akavimega, akawapa wanafunzi wake, nao wanafunzi wakawapa makutano.

37. Wakala wote wakashiba; wakayaokota masazo ya vipande vya mikate makanda saba, yamejaa.

38. Nao waliokula walikuwa wanaume elfu nne, bila wanawake na watoto.

39. Akawaaga makutano, akapanda chomboni, akaenda pande za Magadani.

About Mathayo Chapter 15

Read Mathayo Chapter 15 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of Mathayo in the New Testament. Continue reading with the chapter navigation above or explore the complete book.

Book Information

Book: Mathayo
Chapter: 15
Testament: New Testament

How to Read this Chapter

Use the Previous and Next Chapter buttons to continue reading Mathayo. You can also adjust the font size for comfortable reading and browse other books of the Bible using the navigation links.

https://www.youtube.com/watch?v=rzsT_Q3KLzE

More Resources

Continue Reading the Bible

Continue reading Mathayo Chapter 15 and explore every book, chapter and verse of the Holy Bible. Use the navigation links above and below to move through the Scriptures with ease.

Frequently Asked Questions

What is Mathayo Chapter 15?

Mathayo Chapter 15 is part of the Book of Mathayo in the Holy Bible.

Can I read this chapter online?

Yes. You can read the complete Mathayo Chapter 15 online for free with easy chapter navigation.

More Chapters from Agano Jipya

  1. Waebrania Chapter 1
  2. Waebrania Chapter 5
  3. Waebrania Chapter 6
  4. Waebrania Chapter 4
  5. Waebrania Chapter 3
  6. Waebrania Chapter 2
  7. Yohana Chapter 1

Explore More from mathayo

  1. Mathayo Chapter 16
  2. Mathayo Chapter 17
  3. Mathayo Chapter 8
  4. Mathayo Chapter 19
  5. Mathayo Chapter 27
  6. Mathayo Chapter 11
  7. Mathayo Chapter 18

Related Chapters & Readings

  1. Mambo ya Walawi Chapter 11
  2. Zaburi Chapter 30
  3. Mathayo Chapter 28
  4. 1 Mambo ya Nyakati Chapter 20
  5. 1 Samweli Chapter 13
  6. Ezekieli Chapter 42
  7. Zekaria Chapter 6
Share Your Love

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *