Read Mathayo Chapter 20 Online
Read Mathayo Chapter 20 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of Mathayo in the New Testament. Browse every verse with easy chapter navigation, continue to the next chapter, or explore the complete Book of Mathayo and the Holy Bible online.
Choose a Chapter
Mathayo 20
Sura 20
1. Kwa maana ufalme wa mbinguni umefanana na mtu mwenye nyumba aliyetoka alfajiri kwenda kuajiri wakulima awapeleke katika shamba lake la mizabibu.
2. Naye alipokwisha kupatana na wakulima kuwapa kutwa dinari, aliwapeleka katika shamba lake la mizabibu.
3. Akatoka mnamo saa tatu, akaona wengine wamesimama sokoni wasiokuwa na kazi;
4. na hao nao akawaambia, Enendeni nanyi katika shamba langu la mizabibu, na iliyo haki nitawapa. Wakaenda.
5. Akatoka tena mnamo saa sita na saa kenda, akafanya vile vile.
6. Hata kama saa kumi na moja akatoka, akakuta wengine wamesimama, akawaambia, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi?
7. Wakamwambia, Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Akawaambia, enendeni nanyi katika shamba la mizabibu.
8. Kulipokuchwa, yule bwana wa shamba akamwambia msimamizi wake, Waite wakulima, uwalipe ujira wao, ukianzia wa mwisho hata wa kwanza.
9. Na walipokuja wale wa saa kumi na moja, walipokea kila mtu dinari.
10. Na wale wa kwanza walipokuja, walidhani kwamba watapokea zaidi; na hao pia wakapokea kila mtu dinari.
11. Basi wakiisha kuipokea, wakamnung'unikia mwenye nyumba,
12. wakisema, Hao wa mwisho wametenda kazi saa moja tu, nawe umewasawazisha na sisi tuliostahimili taabu na hari za mchana kutwa.
13. Naye akamjibu mmoja wao, akamwambia, Rafiki, sikudhulumu; hukupatana nami kwa dinari?
14. Chukua iliyo yako, uende zako; napenda kumpa huyu wa mwisho sawa na wewe.
15. Si halali yangu kutumia vilivyo vyangu kama nipendavyo? Au jicho lako limekuwa ovu kwa sababu ya mimi kuwa mwema?
16. Vivyo hivyo wa mwisho watakuwa wa kwanza, na wa kwanza watakuwa wa mwisho.
17. Hata Yesu alipokuwa akipanda kwenda Yerusalemu, aliwachukua wale wanafunzi kumi na wawili faraghani; na njiani akawaambia,
18. Angalieni, tunapanda kwenda Yerusalemu; na Mwana wa Adamu atatiwa mikononi mwa wakuu wa makuhani na waandishi; nao watamhukumu afe;
19. kisha watampeleka kwa Mataifa wapate kumdhihaki, na kumpiga mijeledi, na kumsulibisha; na siku ya tatu atafufuka.
20. Ndipo mama yao wana wa Zebedayo akamwendea pamoja na wanawe, akamsujudia, na kumwomba neno.
21. Akamwambia, Wataka nini? Akamwambia, Agiza kwamba hawa wanangu wawili waketi mmoja mkono wako wa kuume, na mmoja mkono wako wa kushoto, katika ufalme wako.
22. Yesu akajibu akasema, Hamjui mnaloliomba. Je! Mwaweza kunywea kikombe nitakachonywea mimi? Wakamwambia, Twaweza.
23. Akawaambia, Hakika mtakinywea kikombe changu; lakini kuketi mkono wangu wa kuume na mkono wangu wa kushoto, sina amri kuwapa, bali watapewa waliowekewa tayari na Baba yangu.
24. Na wale kumi waliposikia, waliwakasirikia wale ndugu wawili.
25. Lakini Yesu akawaita, akasema, Mwajua ya kuwa wakuu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu, na wakubwa wao huwatumikisha.
26. Lakini haitakuwa hivyo kwenu; bali mtu ye yote anayetaka kuwa mkubwa kwenu, na awe mtumishi wenu;
27. na mtu ye yote anayetaka kuwa wa kwanza kwenu na awe mtumwa wenu;
28. kama vile Mwana wa Adamu asivyokuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi.
29. Hata walipokuwa wakitoka Yeriko mkutano mkubwa wakamfuata.
30. Na tazama, vipofu wawili wameketi kando ya njia, nao waliposikia ya kwamba Yesu anapita, walipaza sauti, wakisema, Uturehemu, Bwana, mwana wa Daudi!
31. Mkutano wakawakaripia, wanyamaze. Lakini wao wakazidi kupaza sauti, wakisema, Uturehemu, Bwana, mwana wa Daudi!
32. Yesu akasimama, akawaita, akasema, Mnataka niwafanyie nini?
33. Wakamwambia, Bwana, twataka macho yetu yafumbuliwe.
34. Yesu akawahurumia, akawagusa macho yao; mara wakapata kuona, wakamfuata.
About Mathayo Chapter 20
Read Mathayo Chapter 20 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of Mathayo in the New Testament. Continue reading with the chapter navigation above or explore the complete book.
Book Information
Book: Mathayo
Chapter: 20
Testament: New Testament
How to Read this Chapter
Use the Previous and Next Chapter buttons to continue reading Mathayo. You can also adjust the font size for comfortable reading and browse other books of the Bible using the navigation links.
More Resources
Continue Reading the Bible
Continue reading Mathayo Chapter 20 and explore every book, chapter and verse of the Holy Bible. Use the navigation links above and below to move through the Scriptures with ease.
Frequently Asked Questions
What is Mathayo Chapter 20?
Mathayo Chapter 20 is part of the Book of Mathayo in the Holy Bible.
Can I read this chapter online?
Yes. You can read the complete Mathayo Chapter 20 online for free with easy chapter navigation.
More Chapters from Agano Jipya
- Waebrania Chapter 1
- Waebrania Chapter 5
- Waebrania Chapter 6
- Waebrania Chapter 4
- Waebrania Chapter 2
- Ufunuo wa Yohana Chapter 15
- Ufunuo wa Yohana Chapter 8
Explore More from mathayo
- Mathayo Chapter 23
- Mathayo Chapter 9
- Mathayo Chapter 10
- Mathayo Chapter 4
- Mathayo Chapter 14
- Mathayo Chapter 7
- Mathayo Chapter 1