Waebrania Chapter 13

For English

Read Waebrania Chapter 13 Online

Read Waebrania Chapter 13 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of Waebrania in the New Testament. Browse every verse with easy chapter navigation, continue to the next chapter, or explore the complete Book of Waebrania and the Holy Bible online.

Choose a Chapter

Waebrania 13

Sura 13

1. Upendano wa ndugu na udumu.

2. Msisahau kuwafadhili wageni; maana kwa njia hii wengine wamewakaribisha malaika pasipo kujua.

3. Wakumbukeni hao waliofungwa kana kwamba mmefungwa pamoja nao; na hao wanaodhulumiwa, kwa vile ninyi nanyi mlivyo katika mwili.

4. Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu.

5. Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa.

6. Hata twathubutu kusema, Bwana ndiye anisaidiaye, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?

7. Wakumbukeni wale waliokuwa wakiwaongoza, waliowaambia neno la Mungu; tena, kwa kuuchunguza sana mwisho wa mwenendo wao, iigeni imani yao.

8. Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele.

9. Msichukuliwe na mafundisho ya namna nyingine nyingine, na ya kigeni; maana ni vizuri moyo ufanywe imara kwa neema, wala si kwa vyakula, ambavyo wao waliokwenda navyo hawakupata faida.

10. Tuna madhabahu ambayo wale waihudumiao ile hema hawana ruhusa kula vitu vyake.

11. Maana wanyama wale ambao damu yao huletwa ndani ya patakatifu na kuhani mkuu kwa ajili ya dhambi, viwiliwili vyao huteketezwa nje ya kambi.

12. Kwa ajili hii Yesu naye, ili awatakase watu kwa damu yake mwenyewe, aliteswa nje ya lango.

13. Basi na tutoke tumwendee nje ya kambi, tukichukua shutumu lake.

14. Maana hapa hatuna mji udumuo, bali twautafuta ule ujao.

15. Basi, kwa njia yake yeye, na tumpe Mungu dhabihu ya sifa daima, yaani, tunda la midomo iliungamayo jina lake.

16. Lakini msisahau kutenda mema na kushirikiana; maana sadaka kama hizi ndizo zimpendezazo Mungu.

17. Watiini wenye kuwaongoza, na kuwanyenyekea; maana wao wanakesha kwa ajili ya roho zenu, kama watu watakaotoa hesabu, ili kwamba wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi.

18. Tuombeeni; maana tunaamini kwamba tuna dhamiri njema, tukitaka kuwa na mwenendo mwema katika mambo yote.

19. Nami nawasihi zaidi sana kufanya hayo ili nirudishwe kwenu upesi.

20. Basi, Mungu wa amani aliyemleta tena kutoka kwa wafu Mchungaji Mkuu wa kondoo, kwa damu ya agano la milele, yeye Bwana wetu Yesu,

21. awafanye ninyi kuwa wakamilifu katika kila tendo jema, mpate kuyafanya mapenzi yake, naye akifanya ndani yetu lipendezalo mbele zake, kwa Yesu Kristo; utukufu una yeye milele na milele. Amina.

22. Lakini nawasihi, ndugu, mchukuliane na neno hili lenye maonyo maana nimewaandikia kwa maneno machache.

23. Jueni ya kuwa ndugu yetu Timotheo amekwisha kufunguliwa; ambaye, akija upesi, nitaonana nanyi pamoja naye.

24. Wasalimuni wote wenye kuwaongoza, na watakatifu wote; hao walio wa Italia wanawasalimu.

25. Neema na iwe nanyi nyote.

About Waebrania Chapter 13

Read Waebrania Chapter 13 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of Waebrania in the New Testament. Continue reading with the chapter navigation above or explore the complete book.

Book Information

Book: Waebrania
Chapter: 13
Testament: New Testament

How to Read this Chapter

Use the Previous and Next Chapter buttons to continue reading Waebrania. You can also adjust the font size for comfortable reading and browse other books of the Bible using the navigation links.

https://www.youtube.com/watch?v=rzsT_Q3KLzE

More Resources

Continue Reading the Bible

Continue reading Waebrania Chapter 13 and explore every book, chapter and verse of the Holy Bible. Use the navigation links above and below to move through the Scriptures with ease.

Frequently Asked Questions

What is Waebrania Chapter 13?

Waebrania Chapter 13 is part of the Book of Waebrania in the Holy Bible.

Can I read this chapter online?

Yes. You can read the complete Waebrania Chapter 13 online for free with easy chapter navigation.

More Chapters from Agano Jipya

  1. Waebrania Chapter 1
  2. Waebrania Chapter 5
  3. Waebrania Chapter 6
  4. Waebrania Chapter 4
  5. Ufunuo wa Yohana Chapter 15
  6. Ufunuo wa Yohana Chapter 8
  7. Ufunuo wa Yohana Chapter 1

Explore More from waebrania

  1. Waebrania Chapter 12
  2. Waebrania Chapter 2
  3. Waebrania Chapter 3
  4. Waebrania Chapter 11
  5. Waebrania Chapter 5
  6. Waebrania Chapter 4
  7. Waebrania Chapter 9

Related Chapters & Readings

  1. 1 Mambo ya Nyakati Chapter 9
  2. Matendo ya Mitume Chapter 23
  3. Matendo ya Mitume Chapter 14
  4. Yohana Chapter 13
  5. Yohana Chapter 21
  6. Ezra Chapter 8
  7. Ezekieli Chapter 38
Share Your Love

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *