Ufunuo wa Yohana Chapter 8

For English

Read Ufunuo wa Yohana Chapter 8 Online

Read Ufunuo wa Yohana Chapter 8 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of Ufunuo wa Yohana in the New Testament. Browse every verse with easy chapter navigation, continue to the next chapter, or explore the complete Book of Ufunuo wa Yohana and the Holy Bible online.

Choose a Chapter

Ufunuo wa Yohana 8

Sura 8

1. Hata alipoifungua muhuri ya saba, kukawa kimya mbinguni kama muda wa nusu saa.

2. Nami nikawaona wale malaika saba wasimamao mbele za Mungu, nao wakapewa baragumu saba.

3. Na malaika mwingine akaja akasimama mbele ya madhabahu, mwenye chetezo cha dhahabu, akapewa uvumba mwingi, ili autie pamoja na maombi ya watakatifu wote juu ya madhabahu ya dhahabu, iliyo mbele ya kiti cha enzi.

4. Na moshi wa ule uvumba ukapanda mbele za Mungu pamoja na maombi ya watakatifu, kutoka mkononi mwa malaika.

5. Na huyo malaika akakitwaa kile chetezo, akakijaza moto wa madhabahu, akautupa juu ya nchi, kukawa radi na sauti na umeme na tetemeko la nchi.

6. Na wale malaika saba wenye baragumu saba wakajifanya tayari ili wazipige.

7. Malaika wa kwanza akapiga baragumu, kukawa mvua ya mawe na moto vilivyotangamana na damu, vikatupwa juu ya nchi; theluthi ya nchi ikateketea, na theluthi ya miti ikateketea, na majani mabichi yote yakateketea.

8. Malaika wa pili akapiga baragumu, na kitu, mfano wa mlima mkubwa uwakao moto, kikatupwa katika bahari; theluthi ya bahari ikawa damu.

9. Wakafa theluthi ya viumbe vilivyomo baharini, vyenye uhai; theluthi ya merikebu zikaharibiwa.

10. Malaika wa tatu akapiga baragumu, nyota kubwa ikaanguka kutoka mbinguni, iliyokuwa ikiwaka kama taa, ikaanguka juu ya theluthi ya mito, na juu ya chemchemi za maji.

11. Na jina lake ile nyota yaitwa Pakanga; theluthi ya maji ikawa pakanga, na wanadamu wengi wakafa kwa maji hayo, kwa kuwa yalitiwa uchungu.

12. Malaika wa nne akapiga baragumu, theluthi ya jua ikapigwa, na theluthi ya mwezi, na theluthi ya nyota, ili kwamba ile theluthi itiwe giza, mchana usiangaze theluthi yake, wala usiku vivyo hivyo.

13. Kisha nikaona, nikasikia tai mmoja akiruka katikati ya mbingu, akisema kwa sauti kuu, Ole, ole, ole wao wakaao juu ya nchi! Kwa sababu ya sauti zisaliazo za baragumu za malaika watatu, walio tayari kupiga.

About Ufunuo wa Yohana Chapter 8

Read Ufunuo wa Yohana Chapter 8 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of Ufunuo wa Yohana in the New Testament. Continue reading with the chapter navigation above or explore the complete book.

Book Information

Book: Ufunuo wa Yohana
Chapter: 8
Testament: New Testament

How to Read this Chapter

Use the Previous and Next Chapter buttons to continue reading Ufunuo wa Yohana. You can also adjust the font size for comfortable reading and browse other books of the Bible using the navigation links.

https://www.youtube.com/watch?v=rzsT_Q3KLzE

More Resources

Continue Reading the Bible

Continue reading Ufunuo wa Yohana Chapter 8 and explore every book, chapter and verse of the Holy Bible. Use the navigation links above and below to move through the Scriptures with ease.

Frequently Asked Questions

What is Ufunuo wa Yohana Chapter 8?

Ufunuo wa Yohana Chapter 8 is part of the Book of Ufunuo wa Yohana in the Holy Bible.

Can I read this chapter online?

Yes. You can read the complete Ufunuo wa Yohana Chapter 8 online for free with easy chapter navigation.

More Chapters from Agano Jipya

  1. Waebrania Chapter 5
  2. Waebrania Chapter 1
  3. Waebrania Chapter 6
  4. Waebrania Chapter 4
  5. Ufunuo wa Yohana Chapter 15
  6. Ufunuo wa Yohana Chapter 1
  7. Waebrania Chapter 11

Explore More from ufunuo-wa-yohana

  1. Ufunuo wa Yohana Chapter 19
  2. Ufunuo wa Yohana Chapter 5
  3. Ufunuo wa Yohana Chapter 21
  4. Ufunuo wa Yohana Chapter 9
  5. Ufunuo wa Yohana Chapter 7
  6. Ufunuo wa Yohana Chapter 18
  7. Ufunuo wa Yohana Chapter 6

Related Chapters & Readings

  1. Ezekieli Chapter 42
  2. Waebrania Chapter 4
  3. Ayubu Chapter 20
  4. Nehemia Chapter 10
  5. 1 Wafalme Chapter 3
  6. Yohana Chapter 10
  7. Kutoka Chapter 8
Share Your Love

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *