Mithali Chapter 29

For English

Read Mithali Chapter 29 Online

Read Mithali Chapter 29 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of Mithali in the Old Testament. Browse every verse with easy chapter navigation, continue to the next chapter, or explore the complete Book of Mithali and the Holy Bible online.

Choose a Chapter

Mithali 29

Sura 29

1. Aonywaye mara nyingi akishupaza shingo, Atavunjika ghafula, wala hapati dawa.

2. Wenye haki wakiwa na amri, watu hufurahi; Bali mwovu atawalapo, watu huugua.

3. Apendaye hekima humfurahisha babaye; Bali ashikamanaye na makahaba hutapanya mali.

4. Mfalme huithibitisha nchi kwa hukumu; Bali yeye apokeaye rushwa huipindua.

5. Mwenye kujipendekeza kwa jirani yake, Hutandika wavu ili kuitega miguu yake.

6. Kuna mtego katika kosa la mtu mbaya; Bali mwenye haki huimba na kufurahi.

7. Mwenye haki huyaangalia madai ya maskini; Bali mtu mbaya hana ufahamu hata ayajue.

8. Watu wenye dharau huwasha mji moto; Bali wenye hekima hugeuzia mbali ghadhabu.

9. Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu; Akikasirika au akicheka, pia hapana raha.

10. Wamwagao damu humchukia mtu mkamilifu; Bali wenye haki humtunza nafsi yake.

11. Mpumbavu hudhihirisha hasira yake yote; Bali mwenye hekima huizuia na kuituliza.

12. Mwenye kutawala akisikiliza uongo; Basi watumishi wake wote watakuwa waovu.

13. Maskini na mdhalimu hukutana pamoja; Bwana huwatia nuru macho yao wote wawili.

14. Mfalme awahukumuye maskini kwa uaminifu; Kiti chake cha enzi kitathibitika milele.

15. Fimbo na maonyo hutia hekima; Bali mwana aliyeachiliwa humwaibisha mamaye.

16. Waovu wakiongezeka, maasi huongezeka; Bali wenye haki watayatazama maanguko yao.

17. Mrudi mwanao naye atakustarehesha; Naam, atakufurahisha nafsi yako.

18. Pasipo maono, watu huacha kujizuia; Bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.

19. Haitoshi mtumwa kuonywa kwa maneno; Maana ajapoyafahamu hataitika.

20. Je! Umemwona mtu mwenye kuhamaki katika maneno? Afadhali kumtumaini mpumbavu kuliko yeye.

21. Amtunduiaye mtumwa wake tangu utoto, Mwisho wake atakuwa ni mwanawe.

22. Mtu wa hasira huchochea ugomvi; Na mtu mwenye ghadhabu huasi sana.

23. Kiburi cha mtu kitamshusha; Bali mwenye roho ya unyenyekevu ataheshimiwa.

24. Mshiriki wa mwivi huichukia nafsi yake mwenyewe; Asikia maapizo, wala hana neno.

25. Kuwaogopa wanadamu huleta mtego; Bali amtumainiye Bwana atakuwa salama.

26. Watu wengi hutafuta upendeleo wa mkuu; Bali hukumu ya kila mtu hutoka kwa Bwana

27. Mtu aliye dhalimu ni chukizo kwa wenye haki; Na mnyofu wa mwenendo ni chukizo kwa waovu.

About Mithali Chapter 29

Read Mithali Chapter 29 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of Mithali in the Old Testament. Continue reading with the chapter navigation above or explore the complete book.

Book Information

Book: Mithali
Chapter: 29
Testament: Old Testament

How to Read this Chapter

Use the Previous and Next Chapter buttons to continue reading Mithali. You can also adjust the font size for comfortable reading and browse other books of the Bible using the navigation links.

https://www.youtube.com/watch?v=rzsT_Q3KLzE

More Resources

Continue Reading the Bible

Continue reading Mithali Chapter 29 and explore every book, chapter and verse of the Holy Bible. Use the navigation links above and below to move through the Scriptures with ease.

Frequently Asked Questions

What is Mithali Chapter 29?

Mithali Chapter 29 is part of the Book of Mithali in the Holy Bible.

Can I read this chapter online?

Yes. You can read the complete Mithali Chapter 29 online for free with easy chapter navigation.

More Chapters from Agano la Kale

  1. Zaburi Chapter 1
  2. Habakuki Chapter 3
  3. Ayubu Chapter 1
  4. Zaburi Chapter 2
  5. Kutoka Chapter 11
  6. Kutoka Chapter 2
  7. Ayubu Chapter 4

Explore More from mithali

  1. Mithali Chapter 3
  2. Mithali Chapter 21
  3. Mithali Chapter 27
  4. Mithali Chapter 11
  5. Mithali Chapter 30
  6. Mithali Chapter 25
  7. Mithali Chapter 9

Related Chapters & Readings

  1. Luka Chapter 10
  2. Isaya Chapter 49
  3. Isaya Chapter 59
  4. Maombolezo Chapter 1
  5. 2 Wafalme Chapter 6
  6. Hosea Chapter 6
  7. 2 Wakorintho Chapter 6
Share Your Love

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *