Read Mithali Chapter 21 Online
Read Mithali Chapter 21 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of Mithali in the Old Testament. Browse every verse with easy chapter navigation, continue to the next chapter, or explore the complete Book of Mithali and the Holy Bible online.
Choose a Chapter
Mithali 21
Sura 21
1. Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa Bwana; Kama mifereji ya maji huugeuza po pote apendapo.
2. Kila njia ya mtu ni sawa machoni pake mwenyewe; Bali Bwana huipima mioyo.
3. Kutenda haki na hukumu Humpendeza Bwana kuliko kutoa sadaka.
4. Macho yenye kiburi, na moyo wa kutakabari, Hata ukulima wa waovu, ni dhambi.
5. Mawazo ya wenye bidii huuelekea utajiri tu; Bali kila mwenye pupa huuelekea uhitaji.
6. Kupata akiba ya mali kwa ulimi wa uongo Ni moshi upeperushwao; ni kutafuta mauti.
7. Jeuri ya wabaya itawaondolea mbali; Kwa sababu wamekataa kutenda hukumu.
8. Njia yake aliyelemewa na dhambi imepotoka sana; Bali mtu aliye safi, kazi yake ni sawasawa.
9. Ni afadhali kukaa katika pembe ya darini, Kuliko katika nyumba pana pamoja na mwanamke mgomvi.
10. Nafsi ya mtu mbaya hutamani uovu; Jirani yake hapati fadhili machoni pake.
11. Mwenye mzaha aadhibiwapo, mjinga hupata hekima; Na mwenye hekima afundishwapo, hupokea maarifa.
12. Mwenye haki huitafakari nyumba ya mtu mbaya; Jinsi wabaya waangushwavyo wakaangamia.
13. Azibaye masikio yake asisikie kilio cha maskini, Yeye naye atalia, lakini hatasikiwa.
14. Kipawa cha siri hutuliza hasira; Na rushwa bindoni humliza ghadhabu kali.
15. Ni furaha yao wenye haki kutenda hukumu; Lakini ni uharibifu kwao watendao maovu.
16. Mtu aikosaye njia ya busara Atakaa katika mkutano wao waliokufa.
17. Mtu apendaye anasa atakuwa maskini; Apendaye mvinyo na mafuta hatakuwa tajiri.
18. Mtu asiye haki ni fidia ya wenye haki; Naye afanyaye hila ni badala ya watu wa adili.
19. Ni afadhali kukaa katika nchi ya nyika; Kuliko na mwanamke mgomvi, mchokozi.
20. Kuna hazina ya thamani na mafuta katika maskani ya mwenye hekima; Bali mwanadamu aliye mpumbavu huyameza.
21. Aandamaye haki na fadhili, Ataona uhai na haki na heshima.
22. Mwenye hekima huupandia mji wao wenye nguvu; Na kuziangusha nguvu za tumaini lao.
23. Mtu azuiaye kinywa chake na ulimi wake, Atajilinda nafsi yake na taabu.
24. Mwenye kiburi na kutakabari, jina lake ni mbishi; Hutenda mambo katika majivuno ya kiburi chake.
25. Matakwa yake mtu mvivu humfisha, Kwa maana mikono yake hukataa kufanya kazi.
26. Kuna atamaniye kwa choyo mchana kutwa; Bali mwenye haki hutoa wala hanyimi.
27. Sadaka ya wasio haki ni chukizo; Si zaidi sana ailetapo mwenye nia mbaya!
28. Shahidi wa uongo atapotea; Bali mtu asikiaye atasema maneno yadumuyo.
29. Asiye haki huufanya uso wake kuwa mgumu; Bali mtu mnyofu huzifikiri njia zake.
30. Hapana hekima, wala ufahamu, Wala shauri, juu ya Bwana.
31. Farasi huwekwa tayari kwa siku ya vita; Lakini Bwana ndiye aletaye wokovu.
About Mithali Chapter 21
Read Mithali Chapter 21 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of Mithali in the Old Testament. Continue reading with the chapter navigation above or explore the complete book.
Book Information
Book: Mithali
Chapter: 21
Testament: Old Testament
How to Read this Chapter
Use the Previous and Next Chapter buttons to continue reading Mithali. You can also adjust the font size for comfortable reading and browse other books of the Bible using the navigation links.
More Resources
Continue Reading the Bible
Continue reading Mithali Chapter 21 and explore every book, chapter and verse of the Holy Bible. Use the navigation links above and below to move through the Scriptures with ease.
Frequently Asked Questions
What is Mithali Chapter 21?
Mithali Chapter 21 is part of the Book of Mithali in the Holy Bible.
Can I read this chapter online?
Yes. You can read the complete Mithali Chapter 21 online for free with easy chapter navigation.
More Chapters from Agano la Kale
- Zaburi Chapter 1
- Habakuki Chapter 3
- Ayubu Chapter 1
- Zaburi Chapter 2
- Kutoka Chapter 11
- Kutoka Chapter 2
- Ayubu Chapter 4
Explore More from mithali
- Mithali Chapter 7
- Mithali Chapter 10
- Mithali Chapter 17
- Mithali Chapter 9
- Mithali Chapter 5
- Mithali Chapter 4
- Mithali Chapter 24