Mithali Chapter 28

For English

Read Mithali Chapter 28 Online

Read Mithali Chapter 28 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of Mithali in the Old Testament. Browse every verse with easy chapter navigation, continue to the next chapter, or explore the complete Book of Mithali and the Holy Bible online.

Choose a Chapter

Mithali 28

Sura 28

1. Waovu hukimbia wasipofuatiwa na mtu; Bali wenye haki ni wajasiri kama simba.

2. Kwa sababu ya maasi ya nchi wakuu wake huwa wengi; Bali kwa wenye ufahamu na maarifa hali ya nchi hudumishwa

3. Mtu mhitaji awaoneaye maskini, Ni kama mvua ya dhoruba isiyosaza chakula.

4. Wao waiachao sheria huwasifu waovu; Bali wao waishikao hushindana nao.

5. Watu wabaya hawaelewi na hukumu; Bali wamtafutao Bwana huelewa na yote.

6. Afadhali maskini aendaye katika unyofu wake, Kuliko mpotofu wa njia angawa ni tajiri.

7. Yeye aishikaye sheria ni mwana mwenye hekima; Bali aliye rafiki wa walafi humwaibisha babaye.

8. Yeye azidishaye mali yake kwa riba na faida, Humkusanyia mtu awahurumiaye maskini.

9. Yeye aligeuzaye sikio lake asiisikie sheria, Hata sala yake ni chukizo.

10. Kila mtu awapotezaye wenye haki katika njia mbaya, Ataanguka katika rima lake mwenyewe; Bali wakamilifu watarithi mema.

11. Mtu tajiri ana hekima machoni pake mwenyewe; Bali maskini mwenye ufahamu humchunguza sana.

12. Wenye haki washindapo, uko utukufu mwingi; Bali waovu waondokapo, watu hujificha.

13. Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema.

14. Mwanadamu mwenye kicho yu heri sikuzote; Bali mshupavu wa moyo ataangukia madhara.

15. Kama simba angurumaye, na dubu mwenye njaa; Ndivyo alivyo mtu mbaya awatawalaye maskini.

16. Mkuu aliyepungukiwa na akili huwaonea watu sana; Bali achukiaye kutamani ataongeza siku zake.

17. Aliyelemewa na damu ya mtu Atalikimbilia shimo; wala mtu asimzuie.

18. Aendaye kwa unyofu ataokolewa; Bali mkaidi wa njia zake ataanguka mara.

19. Alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele; Bali afuataye mambo ya upuzi atapata umaskini wa kumtosha.

20. Mtu mwaminifu atakuwa na baraka tele; Lakini afanyaye haraka kuwa tajiri hakosi ataadhibiwa.

21. Kupendelea watu si kwema; Wala mtu kuasi kwa ajili ya kipande cha mkate.

22. Mwenye husuda afanya haraka kuwa tajiri; Wala haufikiri uhitaji utakaomjilia.

23. Amkemeaye mwenzake hatimaye atapata kibali; Zaidi ya mtu ajipendekezaye kwa ulimi wake.

24. Aibaye mali ya babaye au mamaye, na kusema, Si kosa; Mwana huyo ni rafiki wa mtu mharibifu.

25. Mwenye nafsi ya kutamani huchochea fitina; Bali amtumainiye Bwana atawandishwa.

26. Mwenye kujitumainia moyo wake ni mjinga; Bali yeye aendaye kwa busara ataokolewa.

27. Mwenye kuwagawia maskini hatahitaji kitu; Bali afichaye macho yake atakuwa na laana nyingi.

28. Wasio haki wainukapo, wanadamu hujificha; Bali waangamiapo, wenye haki huongezeka.

About Mithali Chapter 28

Read Mithali Chapter 28 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of Mithali in the Old Testament. Continue reading with the chapter navigation above or explore the complete book.

Book Information

Book: Mithali
Chapter: 28
Testament: Old Testament

How to Read this Chapter

Use the Previous and Next Chapter buttons to continue reading Mithali. You can also adjust the font size for comfortable reading and browse other books of the Bible using the navigation links.

https://www.youtube.com/watch?v=rzsT_Q3KLzE

More Resources

Continue Reading the Bible

Continue reading Mithali Chapter 28 and explore every book, chapter and verse of the Holy Bible. Use the navigation links above and below to move through the Scriptures with ease.

Frequently Asked Questions

What is Mithali Chapter 28?

Mithali Chapter 28 is part of the Book of Mithali in the Holy Bible.

Can I read this chapter online?

Yes. You can read the complete Mithali Chapter 28 online for free with easy chapter navigation.

More Chapters from Agano la Kale

  1. Zaburi Chapter 1
  2. Habakuki Chapter 3
  3. Ayubu Chapter 1
  4. Zaburi Chapter 2
  5. Ayubu Chapter 4
  6. Kutoka Chapter 11
  7. Kutoka Chapter 2

Explore More from mithali

  1. Mithali Chapter 17
  2. Mithali Chapter 25
  3. Mithali Chapter 21
  4. Mithali Chapter 18
  5. Mithali Chapter 24
  6. Mithali Chapter 31
  7. Mithali Chapter 30

Related Chapters & Readings

  1. Kumbukumbu la Torati Chapter 4
  2. Kumbukumbu la Torati Chapter 25
  3. Warumi Chapter 1
  4. Yeremia Chapter 30
  5. Zaburi Chapter 4
  6. 2 Mambo ya Nyakati Chapter 25
  7. 2 Samweli Chapter 14
Share Your Love

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *