Marko Chapter 16

For English

Read Marko Chapter 16 Online

Read Marko Chapter 16 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of Marko in the New Testament. Browse every verse with easy chapter navigation, continue to the next chapter, or explore the complete Book of Marko and the Holy Bible online.

Choose a Chapter

Marko 16

Sura 16

1. Hata sabato ilipokwisha kupita, Mariamu Magdalene na Mariamu mamaye Yakobo, na Salome walinunua manukato wapate kwenda kumpaka.

2. Hata alfajiri mapema, siku ya kwanza ya juma, wakaenda kaburini, jua lilipoanza kuchomoza;

3. wakasemezana wao kwa wao, Ni nani atakayetuvingirishia lile jiwe mlangoni pa kaburi?

4. Hata walipotazama, waliona ya kuwa lile jiwe limekwisha kuvingirishwa; nalo lilikuwa kubwa mno.

5. Wakaingia kaburini wakaona kijana ameketi upande wa kuume, amevaa vazi jeupe; wakastaajabu.

6. Naye akawaambia, Msistaajabu; mnamtafuta Yesu Mnazareti, aliyesulibiwa; amefufuka; hayupo hapa; patazameni mahali walipomweka.

7. Lakini enendeni zenu, mkawaambie wanafunzi wake, na Petro, ya kwamba awatangulia kwenda Galilaya; huko mtamwona, kama alivyowaambia.

8. Wakatoka nje, wakakimbia kutoka kaburini; kwa maana wameingia tetemeko na ushangao; wala hawakumwambia mtu neno, maana waliogopa. [

9. Naye alipofufuka alfajiri siku ya kwanza ya juma, alimtokea kwanza Mariamu Magdalene, ambaye kwamba alimtoa pepo saba.

10. Huyo akashika njia akawapasha habari wale waliokuwa pamoja naye, nao wakali wanaomboleza na kulia.

11. Walakini hao waliposikia kama yu hai, naye amemwona, hawakusadiki.

12. Baada ya hayo akawatokea watu wawili miongoni mwao, ana sura nyingine; nao walikuwa wakishika njia kwenda shamba.

13. Na hao wakaenda zao wakawapa habari wale wengine; wala hao hawakuwasadiki.

14. Baadaye akaonekana na wale kumi na mmoja walipokuwa wakila, akawakemea kwa kutokuamini kwao na ugumu wa mioyo yao, kwa kuwa hawakuwasadiki wale waliomwona alipofufuka katika wafu.

15. Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.

16. Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa.

17. Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;

18. watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya.

19. Basi Bwana Yesu, baada ya kusema nao, akachukuliwa juu mbinguni, akaketi mkono wa kuume wa Mungu.

20. Nao wale wakatoka, wakahubiri kotekote, Bwana akitenda kazi pamoja nao, na kulithibitisha lile neno kwa ishara zilizofuatana nalo.]

About Marko Chapter 16

Read Marko Chapter 16 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of Marko in the New Testament. Continue reading with the chapter navigation above or explore the complete book.

Book Information

Book: Marko
Chapter: 16
Testament: New Testament

How to Read this Chapter

Use the Previous and Next Chapter buttons to continue reading Marko. You can also adjust the font size for comfortable reading and browse other books of the Bible using the navigation links.

https://www.youtube.com/watch?v=rzsT_Q3KLzE

More Resources

Continue Reading the Bible

Continue reading Marko Chapter 16 and explore every book, chapter and verse of the Holy Bible. Use the navigation links above and below to move through the Scriptures with ease.

Frequently Asked Questions

What is Marko Chapter 16?

Marko Chapter 16 is part of the Book of Marko in the Holy Bible.

Can I read this chapter online?

Yes. You can read the complete Marko Chapter 16 online for free with easy chapter navigation.

More Chapters from Agano Jipya

  1. Waebrania Chapter 1
  2. Waebrania Chapter 5
  3. Waebrania Chapter 6
  4. Waebrania Chapter 4
  5. Waebrania Chapter 3
  6. Waebrania Chapter 2
  7. Yohana Chapter 1

Explore More from Marko

  1. Marko Chapter 6
  2. Marko Chapter 5
  3. Marko Chapter 15
  4. Marko Chapter 11
  5. Marko Chapter 9
  6. Marko Chapter 9
  7. Marko Chapter 4

Related Chapters & Readings

  1. Waamuzi Chapter 1
  2. 2 Petro Chapter 3
  3. Mithali Chapter 14
  4. Isaya Chapter 17
  5. 2 Mambo ya Nyakati Chapter 8
  6. Ezekieli Chapter 2
  7. Ayubu Chapter 27
Share Your Love

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *