Wakolosai Chapter 3

For English

Read Wakolosai Chapter 3 Online

Read Wakolosai Chapter 3 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of Wakolosai in the New Testament. Browse every verse with easy chapter navigation, continue to the next chapter, or explore the complete Book of Wakolosai and the Holy Bible online.

Choose a Chapter

Wakolosai 3

Sura 3

1. Basi mkiwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu Kristo aliko, ameketi mkono wa kuume wa Mungu.

2. Yafikirini yaliyo juu, siyo yaliyo katika nchi.

3. Kwa maana mlikufa, na uhai wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.

4. Kristo atakapofunuliwa, aliye uhai wetu, ndipo na ninyi mtafunuliwa pamoja naye katika utukufu.

5. Basi, vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu;

6. kwa ajili ya mambo hayo huja ghadhabu ya Mungu.

7. Katika hayo ninyi nanyi mlitembea zamani, mlipoishi katika hayo.

8. Lakini sasa yawekeni mbali nanyi haya yote, hasira, na ghadhabu, na uovu, na matukano, na matusi vinywani mwenu.

9. Msiambiane uongo, kwa kuwa mmevua kabisa utu wa kale, pamoja na matendo yake;

10. mkivaa utu mpya, unaofanywa upya upate ufahamu sawasawa na mfano wake yeye aliyeuumba.

11. Hapo hapana Myunani wala Myahudi, kutahiriwa wala kutokutahiriwa, mgeni wala mshenzi, mtumwa wala mwungwana, bali Kristo ni yote, na katika yote.

12. Basi, kwa kuwa mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao, jivikeni moyo wa rehema, utu wema, unyenyekevu, upole, uvumilivu,

13. mkichukuliana, na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake; kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi.

14. Zaidi ya hayo yote jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu.

15. Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu; ndiyo mliyoitiwa katika mwili mmoja; tena iweni watu wa shukrani.

16. Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.

17. Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye.

18. Ninyi wake, watiini waume zenu, kama ipendezavyo katika Bwana.

19. Ninyi waume, wapendeni wake zenu msiwe na uchungu nao.

20. Ninyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote; maana jambo hili lapendeza katika Bwana.

21. Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, wasije wakakata tamaa.

22. Ninyi watumwa, watiini hao ambao kwa mwili ni bwana zenu, katika mambo yote, si kwa utumwa wa macho, kama wajipendekezao kwa wanadamu, bali kwa unyofu wa moyo, mkimcha Bwana.

23. Lo lote mfanyalo, lifanyeni kwa moyo, kama kwa Bwana, wala si kwa wanadamu,

24. mkijua ya kuwa mtapokea kwa Bwana ujira wa urithi. Mnamtumikia Bwana Kristo.

25. Maana adhulumuye atapata mapato ya udhalimu wake, wala hakuna upendeleo.

About Wakolosai Chapter 3

Read Wakolosai Chapter 3 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of Wakolosai in the New Testament. Continue reading with the chapter navigation above or explore the complete book.

Book Information

Book: Wakolosai
Chapter: 3
Testament: New Testament

How to Read this Chapter

Use the Previous and Next Chapter buttons to continue reading Wakolosai. You can also adjust the font size for comfortable reading and browse other books of the Bible using the navigation links.

https://www.youtube.com/watch?v=rzsT_Q3KLzE

More Resources

Continue Reading the Bible

Continue reading Wakolosai Chapter 3 and explore every book, chapter and verse of the Holy Bible. Use the navigation links above and below to move through the Scriptures with ease.

Frequently Asked Questions

What is Wakolosai Chapter 3?

Wakolosai Chapter 3 is part of the Book of Wakolosai in the Holy Bible.

Can I read this chapter online?

Yes. You can read the complete Wakolosai Chapter 3 online for free with easy chapter navigation.

More Chapters from Agano Jipya

  1. Waebrania Chapter 5
  2. Waebrania Chapter 1
  3. Waebrania Chapter 6
  4. Waebrania Chapter 4
  5. Ufunuo wa Yohana Chapter 1
  6. Waebrania Chapter 11
  7. Waebrania Chapter 10

Explore More from wakolosai

  1. Wakolosai Chapter 2
  2. Wakolosai Chapter 1
  3. Wakolosai Chapter 4

Related Chapters & Readings

  1. Luka Chapter 3
  2. Mithali Chapter 12
  3. Ruthu Chapter 1
  4. Ezra Chapter 2
  5. Mwanzo Chapter 28
  6. Mwanzo Chapter 50
  7. Mathayo Chapter 11
Share Your Love

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *