Read 2 Wathesalonike Chapter 2 Online
Read 2 Wathesalonike Chapter 2 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of 2 Wathesalonike in the New Testament. Browse every verse with easy chapter navigation, continue to the next chapter, or explore the complete Book of 2 Wathesalonike and the Holy Bible online.
Choose a Chapter
2 Wathesalonike 2
Sura 2
1. Basi, ndugu, tunakusihini, kwa habari ya kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo, na kukusanyika kwetu mbele zake,
2. kwamba msifadhaishwe upesi hata kuiacha nia yenu, wala msisitushwe, kwa roho, wala kwa neno, wala kwa waraka unaodhaniwa kuwa ni wetu, kana kwamba siku ya Bwana imekwisha kuwapo.
3. Mtu awaye yote asiwadanganye kwa njia yo yote; maana haiji, usipokuja kwanza ule ukengeufu; akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu;
4. yule mpingamizi, ajiinuaye nafsi yake juu ya kila kiitwacho Mungu ama kuabudiwa; hata yeye mwenyewe kuketi katika hekalu la Mungu, akijionyesha nafsi yake kana kwamba yeye ndiye Mungu.
5. Je! Hamkumbuki ya kuwa wakati nilipokuwapo pamoja nanyi naliwaambieni hayo?
6. Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake.
7. Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa.
8. Hapo ndipo atakapofunuliwa yule asi, ambaye Bwana Yesu atamwua kwa pumzi ya kinywa chake, na kumwangamiza kwa ufunuo wa kuwapo kwake;
9. yule ambaye kuja kwake ni kwa mfano wa kutenda kwake Shetani, kwa uwezo wote, na ishara na ajabu za uongo;
10. na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa.
11. Kwa hiyo Mungu awaletea nguvu ya upotevu, wauamini uongo;
12. ili wahukumiwe wote ambao hawakuiamini kweli, bali walikuwa wakijifurahisha katika udhalimu.
13. Lakini imetupasa sisi kumshukuru Mungu sikuzote kwa ajili yenu, ndugu mliopendwa na Bwana, kwa kuwa Mungu amewachagua tangu mwanzo mpate wokovu, katika kutakaswa na Roho, na kuiamini kweli;
14. aliyowaitia ninyi kwa injili yetu, ili kuupata utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo.
15. Basi, ndugu, simameni imara, mkayashike mapokeo mliyofundishwa, ama kwa maneno, ama kwa waraka wetu.
16. Na Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe, na Mungu Baba yetu, aliyetupenda akatupa faraja ya milele na tumaini jema, katika neema,
17. awafariji mioyo yenu, na kuwafanya imara katika kila neno na tendo jema.
About 2 Wathesalonike Chapter 2
Read 2 Wathesalonike Chapter 2 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of 2 Wathesalonike in the New Testament. Continue reading with the chapter navigation above or explore the complete book.
Book Information
Book: 2 Wathesalonike
Chapter: 2
Testament: New Testament
How to Read this Chapter
Use the Previous and Next Chapter buttons to continue reading 2 Wathesalonike. You can also adjust the font size for comfortable reading and browse other books of the Bible using the navigation links.
More Resources
Continue Reading the Bible
Continue reading 2 Wathesalonike Chapter 2 and explore every book, chapter and verse of the Holy Bible. Use the navigation links above and below to move through the Scriptures with ease.
Frequently Asked Questions
What is 2 Wathesalonike Chapter 2?
2 Wathesalonike Chapter 2 is part of the Book of 2 Wathesalonike in the Holy Bible.
Can I read this chapter online?
Yes. You can read the complete 2 Wathesalonike Chapter 2 online for free with easy chapter navigation.
More Chapters from 2 Wathesalonike
Explore More from Agano Jipya
- Warumi Chapter 8
- 1 Wathesalonike Chapter 4
- 2 Timotheo Chapter 1
- 1 Wakorintho Chapter 13
- Mathayo Chapter 11
- Matendo ya Mitume Chapter 20
- Ufunuo wa Yohana Chapter 7