Yohana Chapter 9

For English

Read Yohana Chapter 9 Online

Read Yohana Chapter 9 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of Yohana in the New Testament. Browse every verse with easy chapter navigation, continue to the next chapter, or explore the complete Book of Yohana and the Holy Bible online.

Choose a Chapter

Yohana 9

Sura 9

1. Hata alipokuwa akipita alimwona mtu, kipofu tangu kuzaliwa.

2. Wanafunzi wake wakamwuliza wakisema, Rabi, ni yupi aliyetenda dhambi, mtu huyu au wazazi wake, hata azaliwe kipofu?

3. Yesu akajibu, Huyu hakutenda dhambi, wala wazazi wake; bali kazi za Mungu zidhihirishwe ndani yake.

4. Imetupasa kuzifanya kazi zake yeye aliyenipeleka maadamu ni mchana, usiku waja asipoweza mtu kufanya kazi.

5. Muda nilipo ulimwenguni, mimi ni nuru ya ulimwengu.

6. Alipokwisha kusema hayo, alitema mate chini, akafanya tope kwa yale mate. Akampaka kipofu tope za macho,

7. akamwambia, Nenda kanawe katika birika ya Siloamu, (maana yake, Aliyetumwa). Basi akaenda na kunawa; akarudi anaona.

8. Basi jirani zake, na wale waliomwona zamani kuwa ni mwombaji, wakasema, Je! Huyu siye yule aliyekuwa akiketi na kuomba?

9. Wengine wakasema, Ndiye. Wengine wakasema, La, lakini amefanana naye. Yeye mwenyewe alisema, Mimi ndiye.

10. Basi wakamwambia, Macho yako yalifumbuliwaje?

11. Yeye akajibu, Mtu yule aitwaye Yesu alifanya tope, akanipaka macho akaniambia, Nenda Siloamu ukanawe; basi nikaenda na kunawa, nikapata kuona.

12. Wakamwambia, Yuko wapi huyo? Akasema, Mimi sijui.

13. Basi wakampeleka kwa Mafarisayo yule aliyekuwa kipofu zamani.

14. Nayo ilikuwa sabato, hapo Yesu alipofanya zile tope na kumfumbua macho.

15. Basi Mafarisayo nao wakamwuliza tena jinsi gani alivyopata kuona. Akawaambia, Alinitia tope juu ya macho, nami nikanawa, na sasa naona.

16. Basi baadhi ya Mafarisayo wakasema, Mtu huyo hakutoka kwa Mungu, kwa sababu haishiki sabato. Wengine wakasema, Awezaje mtu mwenye dhambi kufanya ishara kama hizo? Kukawa matengano kati yao.

17. Basi wakamwambia yule kipofu mara ya pili, Wewe wasemaje katika habari zake kwa vile alivyokufumbua macho? Akasema, Ni nabii.

18. Basi Wayahudi hawakusadiki habari zake, ya kuwa alikuwa kipofu, kisha akapata kuona; hata walipowaita wazazi wake yule aliyepata kuona.

19. Wakawauliza wakisema, Huyu ndiye mwana wenu, ambaye mnasema kwamba alizaliwa kipofu? Amepataje, basi, kuona sasa?

20. Wazazi wake wakawajibu, wakasema, Tunajua ya kuwa huyu ndiye mwana wetu, tena ya kuwa alizaliwa kipofu;

21. lakini jinsi aonavyo sasa hatujui; wala hatujui ni nani aliyemfumbua macho. Mwulizeni yeye mwenyewe; yeye ni mtu mzima; atajisemea mwenyewe.

22. Wazazi wake waliyasema hayo kwa sababu waliwaogopa Wayahudi; kwa maana Wayahudi walikuwa wamekwisha kuafikiana kwamba mtu akimkiri kuwa ni Kristo, atatengwa na sinagogi.

23. Ndiyo sababu wale wazazi wake walisema, Ni mtu mzima, mwulizeni yeye.

24. Basi mara ya pili wakamwita yule mtu aliyekuwa kipofu, wakamwambia, Mpe Mungu utukufu. Sisi tunajua ya kuwa mtu huyo ni mwenye dhambi.

25. Basi yule mtu akajibu, Kwamba yeye ni mwenye dhambi sijui. Najua neno moja, kuwa mimi nalikuwa kipofu na sasa naona.

26. Basi wakamwambia, Alikutendea nini? Alikufumbua macho jinsi gani?

27. Akawajibu, Nimekwisha kuwaambia, wala hamkusikia; mbona mnataka kusikia tena? Ninyi nanyi mnataka kuwa wanafunzi wake?

28. Basi wakamshutumu, wakasema, Wewe u mwanafunzi wake yule; sisi tu wanafunzi wa Musa.

29. Sisi tunajua ya kuwa Mungu alisema na Musa; bali yule hatujui atokako.

30. Yule mtu akajibu, akawaambia, Hii ni ajabu! Kwamba ninyi hamjui atokako, naye alinifumbua macho!

31. Twajua ya kuwa Mungu hawasikii wenye dhambi; bali mtu akiwa ni mcha Mungu, na kuyafanya mapenzi yake, humsikia huyo.

32. Tokea hapo haijasikiwa ya kuwa mtu ameyafumbua macho ya kipofu, ambaye alizaliwa hali hiyo.

33. Kama huyo asingalitoka kwa Mungu, asingeweza kutenda neno lo lote.

34. Wakajibu, wakamwambia, Ama! Wewe ulizaliwa katika dhambi tupu, nawe unatufundisha sisi? Wakamtoa nje.

35. Yesu akasikia kwamba wamemtoa nje; naye alipomwona alisema, Wewe wamwamini Mwana wa Mungu?

36. Naye akajibu akasema, Ni nani, Bwana, nipate kumwamini?

37. Yesu akamwambia, Umemwona, naye anayesema nawe ndiye.

38. Akasema, Naamini, Bwana. Akamsujudia.

39. Yesu akasema, Mimi nimekuja ulimwenguni humu kwa hukumu, ili wao wasioona waone, nao wanaoona wawe vipofu.

40. Baadhi ya Mafarisayo waliokuwapo pamoja naye wakasikia hayo, wakamwambia, Je! Sisi nasi tu vipofu?

41. Yesu akawaambia, Kama mngekuwa vipofu, msingekuwa na dhambi; lakini sasa mwasema, Twaona; basi dhambi yenu inakaa.

About Yohana Chapter 9

Read Yohana Chapter 9 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of Yohana in the New Testament. Continue reading with the chapter navigation above or explore the complete book.

Book Information

Book: Yohana
Chapter: 9
Testament: New Testament

How to Read this Chapter

Use the Previous and Next Chapter buttons to continue reading Yohana. You can also adjust the font size for comfortable reading and browse other books of the Bible using the navigation links.

https://www.youtube.com/watch?v=rzsT_Q3KLzE

More Resources

Continue Reading the Bible

Continue reading Yohana Chapter 9 and explore every book, chapter and verse of the Holy Bible. Use the navigation links above and below to move through the Scriptures with ease.

Frequently Asked Questions

What is Yohana Chapter 9?

Yohana Chapter 9 is part of the Book of Yohana in the Holy Bible.

Can I read this chapter online?

Yes. You can read the complete Yohana Chapter 9 online for free with easy chapter navigation.

More Chapters from Agano Jipya

  1. Waebrania Chapter 5
  2. Waebrania Chapter 1
  3. Waebrania Chapter 6
  4. Waebrania Chapter 4
  5. Ufunuo wa Yohana Chapter 1
  6. Waebrania Chapter 11
  7. Waebrania Chapter 10

Explore More from yohana

  1. Yohana Chapter 16
  2. Yohana Chapter 12
  3. Yohana Chapter 1
  4. Yohana Chapter 5
  5. Yohana Chapter 20
  6. Yohana Chapter 11
  7. Yohana Chapter 17

Related Chapters & Readings

  1. Amosi Chapter 2
  2. Luka Chapter 12
  3. Mambo ya Walawi Chapter 11
  4. Nehemia Chapter 3
  5. Mwanzo Chapter 10
  6. Ezekieli Chapter 21
  7. 2 Yohana Chapter 1
Share Your Love

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *