Wagalatia Chapter 6

For English

Read Wagalatia Chapter 6 Online

Read Wagalatia Chapter 6 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of Wagalatia in the New Testament. Browse every verse with easy chapter navigation, continue to the next chapter, or explore the complete Book of Wagalatia and the Holy Bible online.

Choose a Chapter

Wagalatia 6

Sura 6

1. Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lo lote, ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole, ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe.

2. Mchukuliane mizigo na kuitimiza hivyo sheria ya Kristo.

3. Maana mtu akijiona kuwa ni kitu, naye si kitu, ajidanganya nafsi yake.

4. Lakini kila mtu na aipime kazi yake mwenyewe, ndipo atakapokuwa na sababu ya kujisifu ndani ya nafsi yake tu, wala si kwa mwenzake.

5. Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe.

6. Mwanafunzi na amshirikishe mkufunzi wake katika mema yote.

7. Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa cho chote apandacho mtu, ndicho atakachovuna.

8. Maana yeye apandaye kwa mwili wake, katika mwili wake atavuna uharibifu; bali yeye apandaye kwa Roho, katika Roho atavuna uzima wa milele.

9. Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho.

10. Kwa hiyo kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema; na hasa jamaa ya waaminio.

11. Tazameni ni kwa herufi gani kubwa nimewaandikia kwa mkono wangu mimi mwenyewe!

12. Wote watakao kuonekana ni wazuri kwa mambo ya mwili, ndio wanaowashurutisha kutahiriwa; makusudi wasiudhiwe kwa ajili ya msalaba wa Kristo, hilo tu.

13. Kwa maana hata wao wenyewe waliotahiriwa hawaishiki sheria; bali wanataka ninyi mtahiriwe, wapate kuona fahari katika miili yenu.

14. Lakini mimi, hasha, nisione fahari juu ya kitu cho chote ila msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambao kwa huo ulimwengu umesulibishwa kwangu, na mimi kwa ulimwengu.

15. Kwa sababu kutahiriwa si kitu, wala kutokutahiriwa, bali kiumbe kipya.

16. Na wote watakaoenenda kwa kanuni hiyo, amani na iwe kwao na rehema, naam, kwa Israeli wa Mungu.

17. Tangu sasa mtu asinitaabishe; kwa maana ninachukua mwilini mwangu chapa zake Yesu.

18. Ndugu zangu, neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja na roho zenu. Amina.

About Wagalatia Chapter 6

Read Wagalatia Chapter 6 online from the Holy Bible. This chapter is part of the Book of Wagalatia in the New Testament. Continue reading with the chapter navigation above or explore the complete book.

Book Information

Book: Wagalatia
Chapter: 6
Testament: New Testament

How to Read this Chapter

Use the Previous and Next Chapter buttons to continue reading Wagalatia. You can also adjust the font size for comfortable reading and browse other books of the Bible using the navigation links.

https://www.youtube.com/watch?v=rzsT_Q3KLzE

More Resources

Continue Reading the Bible

Continue reading Wagalatia Chapter 6 and explore every book, chapter and verse of the Holy Bible. Use the navigation links above and below to move through the Scriptures with ease.

Frequently Asked Questions

What is Wagalatia Chapter 6?

Wagalatia Chapter 6 is part of the Book of Wagalatia in the Holy Bible.

Can I read this chapter online?

Yes. You can read the complete Wagalatia Chapter 6 online for free with easy chapter navigation.

More Chapters from Agano Jipya

  1. Waebrania Chapter 5
  2. Waebrania Chapter 1
  3. Waebrania Chapter 6
  4. Waebrania Chapter 4
  5. Ufunuo wa Yohana Chapter 1
  6. Waebrania Chapter 11
  7. Waebrania Chapter 10

Explore More from wagalatia

  1. Wagalatia Chapter 1
  2. Wagalatia Chapter 4
  3. Wagalatia Chapter 5
  4. Wagalatia Chapter 2
  5. Wagalatia Chapter 3

Related Chapters & Readings

  1. Zaburi Chapter 90
  2. Isaya Chapter 25
  3. Yoeli Chapter 1
  4. Kumbukumbu la Torati Chapter 10
  5. Kutoka Chapter 32
  6. Marko Chapter 13
  7. Zaburi Chapter 24
Share Your Love

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *